Wawakilishi wa katoliki wathibitisha chanjo ya pepo punda ina kemikali inayoathiri uzazi
11th November, 2014
Maswali yanazidi kuongezeka nchini kuhusu madai ya kanisa katoliki kwamba chanjo inayotolewa nchini dhidi ya maradhi ya pepo punda inaendeleza njama fiche. Wawakilishi wa kanisa hilo wamefika mbele ya kamati ya bunge kuhusu afya na kushikilia kauli zao kwamba watafiti wao wamethibitisha kwamba chanjo hiyo ina kemikali inayoathiri uzazi