Wasichana Garissa wanahofia iwapo wanajiunga na kikosi cha NYS, huenda wakakosa kuolewa
9th November, 2014
Mtoto wa kike ni kama ambari na dhahabu katika jamii yetu, na hatukubali wao kujiunga na kikosi cha maafisa wa NYS. Hii ndio kauli ya baadhi ya wazee wa jamiikutoka Garissa baada ya zoezi la kutafuta vijana wa huduma kwa taifa kukosa mtoto wa kike sehemu hio. Baadhi ya wasichana wanahofia iwapo wanajiunga na kikosi hicho, huenda wakakosa kuolewa. Hamza Yusuf anaarifu zaidi.