Seneta Moses Wetangula akumbwa na tatizo la kupumua huko Kisumu
7th November, 2014
Seneta wa Bungoma Moses Wetangula hii leo asubuhi alipelekwa katika hospitali ya aga Khan kisumu baada ya kukumbwa na matatizo ya kupumua. Baada ya kupata habari hizo kwenye mtandao, kinara wa CORD Raila Odinga alimzuru Wetangula katika hospitali hiyo . Daktari mkuu katika hospitali ya agakhan kisumu Sam Oula alisema kwamba Wetangula alikumbwa na tatizo la kupumua ndani ya ndege alipokuwa akisafiri kutoka Nairobi kuelekea kisumu. Hata hivyo alihudumiwa pamoja na kuangaliwa afya yake na madaktari na kisha kuruhusiwa kwenda nyumbani.