Jamii za Wasudan Kusini kudaiwa kuzua uhasama na jamii ya Wakongo
2nd November, 2014
Hali ya wasiwasi imetanda katika kambi ya kakuma sehemu ya turkana baada ya jamii za wasudan kusini kudaiwa kuzua uhasama na kupelekea vita na jamii za warundi na wakongo. Ni vita ambavyo kulingana na maafisa wa polisi vimewaacha watu 8 wamefariki. Kwa sasa wakimbizi wa burundi,kongo na rwanda wamehama makazi yao kambini humo na kukita kambi katika vituo vya polisi na hata makanisani.