Wakenya tisa waliokwama nchini Liberia warejea nchini na kupimwa kuwa salama
29th October, 2014
Wakenya tisa waliokwama nchini Liberia baada ya shirika la ndege la Kenya kusitisha zafari zake nchini humo hatimaye wamerejea nchini. Punde baada ya kutua uwanjani JKIA wakenya hao wamefanyiwa uchunguzi wa virusi vya Ebola na Marburg na kupatikana kuwa salama. Maswali yameanza kuulizwa kuhusu ni kwanini wizara ya afya imeagiza kwamba wakenya hao hawatatangamana na watu kwa muda wa siku 21