Wakenya wanaodhulumiwa kwa kukosa uwakilishi washauriwa jinsi wanavyoweza kufanikiwa kwenye kesi
27th October, 2014
Wakenya wanaodhulumiwa kwa kukosa uwakilishi wa kisheria wamepata fursa ya kushauriwa kuhusu jinsi wanavyoweza kufanikiwa kwenye kesi hizo. Kwenye shughuli iliyoongozwa na jaji mkuu Dkt Willy Mutunga na ambayo pia inafanyika kote nchini, imeibuka kwamba tatizo kuu linalowakumba wakenya kisheria ni suala la ardhi.