Rais Uhuru Kenyatta ataka Mahakama kupewa nafasi ya kutekeleza majukumu yao
18th October, 2014
Rais uhuru Kenyatta na naibu rais William Ruto wanataka mahakama na taasisi zinazohusika na upelelezi kupewa nafasi ya kutekeleza majukumu yao kikamilifu ili kufichua sakata kuhusu umiliki wa ardhi yenye kuzozaniwa katika mtaa wa kifahari wa Karen. Kupitia taarifa kwa vyombo vya habari, msemaji wa ikulu ya rais Manoah Esipisu amesema mtu yetote au afisa wa umma atakayepatikana na makosa ya kuhusika kwa njia moja au nyingine kwenye sakata hiyo ataadhibiwa kwa mujibu wa sheria zilizopo.