Mkenya nchini Marekani afutwa kazi kwa kutembelewa na mwanawe kutoka Kenya
18th October, 2014
Mkenya nchini marekani afutwa kazi kwa kutembelewa na mwanawe kutoka Kenya, akishukiwa kuwa na ugonjwa hatari wa Ebola. Licha ya taifa la Kenya kuwa mbali zaidi kutoka eneo la Afrika magharibi ambako ugonjwa huo umekithiri, Alice anailaumu serikali ya marekani kwa unyanyapaa aliopokea kutokana na kisa hicho.