Wafugaji katika kaunti ya Laikipia kuanza chama cha kuwekeza fedha ili kuwaokoa wakati wa kiangazi
17th October, 2014
Wafugaji hukabiliwa na changamoto nyingi kutokana na desturi za ufugaji zinazowafanya kuhamahama kutafuta malisho. Hali hiyo imewafanya wengi kukosa njia za kuwekeza fedha ili kuwaokoa wakati wa kiangazi mifugo inapokufa. Lakini hali imeanza kubadilika baada ya kundi moja la wafugaji katika kaunti ya Laikipia kuanza chama cha ushirika. Carol Nderi amerejea kutoka Laikipia kaskazini na hii hapa taarifa yake.