"Harambee bado tutafanya" wasisitiza Wabunge licha ya onyo kutolewa na tume ya maadili
14th October, 2014
Kanuni mpya za serikali za kuwakataza maafisa wa serikali kushirikia michango ya harambee zimekosolewa vikali kwenye kikao cha alasiri cha bunge. Wabunge wamesisitiza kuwa wataendelea kushiriki shughuli za kuchangisha fedha licha ya onyo kutolewa na tume ya maadili na kupambana na ufisadi kuwa hatua hiyo ni kinyume cha sheria. Upande wa upinzani umekuwa ukilalama katika siku chache zilizopita kuhusu swala hilo ambalo linasemekana kukiuka sheria ya uongozi na maadili iliyopitishwa mwaka 2012.