Wakaazi wa Old Town Mombasa wahofia kupigwa na hata kuuawa na nguvu za umeme
12th October, 2014
Wakazi wa Old Town Mombasa wameelezea hofu yao kwamba wanaweza kupigwa na hata kuuawa na nguvu za umeme . Hii ni kutokana na kuwa mizizi ya mti mmoja katika eneo hilo imebomoa kibanda cha transfoma na sasa mizizi hiyo inagusana na nyaya za umeme. Kwa sasa wameilaumu kampuni ya Kenya Power kwa kujitia hamnazo licha ya kuarifiwa kuhusu hatari iliyosababishwa na mti huo katika eneo hilo.