Rais Kenyatta atoa wito kwa wakenya kupiga vita matatizo yanayowakumba kama ukosefu wa ajira
9th October, 2014
Mbele ya jumba la Harambee rais Uhuru Kenyatta aliwahutubia mamia ya wakenya waliokuwa wamemsubiri kwa muda wa takriban saa tano akiwa katika msafara wa kutoka uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta. Akiandamana na naibu wa rais William Ruto rais Kenyatta alitoa wito kwa wakenya kuungana ili kuyapiga vita matatizo yanayowakumba kama ukosefu wa ajira miongoni mwa mengine.