IPOA: Polisi walipuuza ripoti za ujasusi kuhusu mavamizi ya Mpeketoni
6th October, 2014
Mamlaka inayosimamia utendakazi wa polisi IPOA, imeikosoa idara ya polisi kwa kile imekitaja kuwa kupuuza ripoti za ujasusi kuhusu mavamizi ya Mpeketoni. Kwenye ripoti maalum kuhusu kisa hicho IPOA inasema kuliwapo taarifa za idara ya ujasusi kuhusu mavamizi hayo ya mwezi Juni. Kama anavyoarifu Ali Manzu, baadhi ya maafisa wa kitengo cha kupambana na magaidi ATPU, wanadaiwa kuwa walishirikiana na wanamgambo wa Al-Shabaab katika kutekeleza maafa hayo.