Wizara ya utalii ya kaunti ya Kwale yaanzisha kampeini ya kuhamasisha shughuli za utalii
30th September, 2014
Wizara ya utalii ya kaunti ya Kwale imeanzisha kampeini ya kuhamasisha shughuli za utalii katika kaunti hiyo. Akizungumza na wanahabari waziri wa utalii na mambo ya mawasiliano ya kiteknolojia Adan Sheikh alisema kuwa wanapania kuanzisha tamasha ya urembo kama mojawapo ya vivutio vitakavyotumika kunadi shughuli za utalii katika kaunti hiyo.