Watu 3 wamefariki kwenye ajali ya barabarani eneo la Athi river, barabara ya Nairobi kulekea Namanga
23rd September, 2014
Walioshuhudia ajali hiyo wamesema, ilitokea baada ya lori lililokuwa likitoka Kitengela kugongana na lori jingine wakati dereva wake alipokuwa akilikwepa gari la kibinafsi lililopunguza kasi ili kuruhusu gari moshi kupita. Dereva alifariki papo hapo huku watu wengine wawili wakifariki walipokuwa wakikimbizwa hospitali. Ajali hiyo ilisababisha msongamano mkubwa wa magari katika barabara kuu ya kutoka Namanga kuelekea Nairobi.