Makabiliano ya risasi yazuka kwenye mkutano wa kupanga kumtimua gavana wa Makueni Kivutha Kibwana
23rd September, 2014
Mlinzi wa gavana wa kaunti ya Makueni Kivutha Kibwana ni miongoni mwa watu 4 waliopigwa risasi katika vurumai iliyokumba mkutano uliopania kumuondoa gavana huyo mamlakani. Maafisa wa polisi waliwajeruhi kwa kuwapiga riasi 4 hao wakati walipowatawanya wenyeji waliokuwa wamefika na gavana Kivuitha Kibwana. Viongozi katika kaunti hiyo wamemtaka gavana Kibwana kuondoka mamlakani kwa kukosa kuwahusisha wenyeji kuhusu ujenzi wa reli, ambao utathiri maisha yao.