×
× KTN KTN News KTN Morning Express KTN Leo Leo Mashinani The Big Story Checkpoint News Center E-Paper Lifestyle & Entertainment Nairobian Entertainment Eve Woman Travelog TV Stations KTN Home KTN News KTN Farmers TV Radio Stations Radio Maisha Spice FM Vybez Radio Enterprise VAS E-Learning Digger Classified Jobs Games Crosswords Sudoku The Standard Group Corporate Contact Us Rate Card Vacancies DCX O.M Portal Corporate Email RMS
Login
×
Show Swahili

Polisi watia nguvuni jamaa watatu waliokuwa wakijifanya kuwa Maafisa wa Polisi

9th September, 2014

Jamaa watatu wanaodaiwa kuhangaisha wenyeji kwa kujifanya kuwa maafisa wa polisi katika eneo la Kivumbini mjini Nakuru wametiwa nguvuni. Watatu hao wanadaiwa kuvaa sare za afisa wa polisi na kuwahangaisha raia katika mitaa ya kivumbini, manyani na kaloleni hususan nyakati za usiku. Naibu wa afisa wa utawala nakuru barnabas kimutai amedai kujuzwa na raia ambao walitamaushwa na jinsi watatu hao walivyokuwa wakiwanyanyasa wenyeji wa eneo hilo . inspekta huyo, amedokeza kuwa polisi wamekuwa wakifanya msako wa wahalifu hao, akidai kuwa mmoja kati ya waliotiwa nguvuni amewahi kuhudumu kama afisa wa polisi. watatu hao wanadaiwa kuwa katika kikundi kijulikanacho kama bongo 4. kwa sasa washukiwa hao wanazuiliwa katika kituo cha polisi cha bondeni mjini nakuru wakisubiri kufanyiwa uchunguzi pamoja na kufunguliwa mashtaka.
.
RELATED VIDEOS