MIGORI COUNTY: Vurumai iliyokuwa katika ziara ya Rais Uhuru Kenyatta yazua hisia mbalimbali
9th September, 2014
Ziara ya Rais Uhuru Kenyatta hapo jana katika kaunti ya migori ilioishia na vurumai imeendelea kuzua hisia mbalimbali miongoni mwa viongozi wa kisiasa. chama cha tna kimekashifu tukio hilo na kukitaka chama cha odm kuomba msamaha kwa vumurai hilo pamoja na kudai kwamba chama hicho kilipanga njama ya kuzua fujo wakati wa hafla hiyo. lakini katika mtazamo tofauti wabunge wa muungano wa cord kutoka kaunti ya migori wamekana kuhusika katika matukio hayo ya kuzomewa kwa rais kenyatta katika ziara yake ya huko Migori.