Wanabiashara Kibera wabadilisha mifupa kuwa mapambo ya thamani
23rd August, 2014
Watu wanaoishi katika mtaa wa mabanda wa Kibera jijini Nairobi wamegundua thamani ya mifupa ya wanyama ambayo aghalabu wewe hung’wafua minofu na kuitupa jaani. Wao wanaisafisha na kuitumia mifupa hiyo kutengeneza mapambo ikiwemo mikufu.