Watu 700 wafariki Sudan Kusini kwa mvutano kati ya Salva Kiir na Riek Machar
22nd August, 2014
Watu zaidi ya mia saba wameuawa nchini Sudan Kusini kwenye mapigano mapya ambayo yamesababishwa na uhasama baina ya Rais wa taifa hilo Salva Kiir na kiongozi wa waasi Riek Machar. Juhudi za kubuni serikali ya mseto hazijafaulu licha ya makataa yaliyowekwa kufikia kikomo.