Busia inatumika kama kiingilio kwa wanaotoroka Ebola nchi za Africa magharibi
20th August, 2014
Afisa mkuu wa afya katika kaunti ya Busia amekariri kuwa watu mia moja, ishirini na wawili wameingia humu nchini kutoka mataifa ya afrika magharibi tangu kutangazwa kuwepo kwa maradhi hayo katika mataifa hayo. Taarifa hii imekinzana ile ya wizara ya maswala ya kigeni iliyowataka wakenya kususia kutoa matamshi yanayolenga kuleta hofu ya maambukizi ya virusi vya Ebola humu nchini