Jamaa akamatwa na kutiwa korokoroni kwa kujifanya polisi na kuitisha hongo ili kusajili makurutu
3rd August, 2014
Inasemekana kuwa mshukiwa huyo kwa jina la Joseph Malai Kaberia amekuwa akiwatoza fedha wakazi wa eneo hilo kwa madai ya kuwasajili kujiunga na taasisi ya mafunzo ya huduma za vijana kwa taifa NYS. Kaberia anayedai wakushirikiana na maafisa fulani wakuu wa polisi wa eneo hilo, alinaswa alipokuwa akiwapa vijana watatu barua za kujiunga na taasisi hiyo, baada ya kuwatoza shilingi laki mbili, na elfu 75. Kamanda wa polisi wa utawala eneo la Igembe kusini Abdi-Rahim Gulia amesema kuwa mshukiwa huyo atafikishwa mahakamani hapo kesho na kufunguliwa mashtaka ya kuhusika na ulaghai.