Wakenya walioleta mabadiliko watuzwa katika tuzo za transform Kenya
20th July, 2014
Tuzo za Transform Kenya Awards zilizoanzishwa na shirika la habari la standard, zitakuwa zikifanyika kila mwaka kwa lengo la kutambua juhudi za watu mbalimbali za kuleta mabadiliko katika jamii. Wakenya tabaka mbalimbali ikiwemo taasisi zilizochangia katika kuleta mabadiliko katika jamii walitambuliwa na kutuzwa kutokana na michango yao muhimu. Benki ya KBC ilitoa ufadhili wa shilingi milioni 15 ili kufanikisha hafla hiyo iliyofanyika katika hoteli ya Windsor.