Kazungu Kambi amewastaafisha Francis Atwoli wa COTU na Jackline Mugo wa FKE
18th July, 2014
Waziri wa Leba Kazungu Kambi amewastaafisha katibu mkuu wa muungano wa wafanyikazi nchini COTU Francis Atwoli na katibu mkuu wa muungano wa waajiri FKE Jackline Mugo kama wanachama katika bodi ya halmashauri ya malipo ya uzeeni NSSF. Kazungu amesema hatua hiyo ni mojawapo ya mageuzi na kuwa wawili hao wamehudumu zaidi ya miaka sita, mda unaohitajika kikatiba. Lakini muda mfupi baada ya waziri Kambi kutangaza mabadiliko hayo, Francis Atwoli aliitisha kikao na wanahabari na kusema kuwa waziri Kambi hana ruhusa na uwezo kikatiba kufanya hivyo na kudai kuwa hii ni njama ya kumnyamazisha baada ya kupuliza kipenga kuhusiana ufisadi unaoendelea katika Halmashauri ya Malipo ya Uzeeni NSSF.