Kenya yakosa kutamba juu ya timu ya Misiri katika mchezo wa Kikapu
16th July, 2014
Timu ya chuo kikuu cha nairobi almaarufu kama terror kinacho wakilisha kenya kwenye mashindano ya vyuo vikuu kilishindwa kutamba dhidi misri na kulazwa kwa tofauti ya alama 3 katika mechi ngumu iliyoandaliwa kwenye ukumbi wa nyao
timu ya terror ilianza robo ya kwanza bila makali na kulazwa 12-17. robo ya pili ubabe wa valentine nyakundi na dan nabuya ukasaidia kenya kutwaa uongozi wa 17-10 na kuenda kwenye mapumziko 29-27 wakenya kifua mbele. baada ya mapumzio james nyaribari akaimarika na kuyakimu mashambulizi ya wamisri kistadi na vuta ni kuvute zao zikikamilisha robo ya tatu 18-14. katika robo ya nne, wakenya wakalegea na abdelaram yosif na karim dahashan wakawagutusha kwa kuipa upande wao alama 14 dhidi ya 5 na kukamilisha mechi52-55 wamisri mbele. upande wa kina dada timu ya u.s.i.u nayo ilizidisha ubabe wao na kufanikiwa kuilaza mozambique kwa alam 46 dhidi ya 42