Vinara wa Cord wamesa hawana haja tena ya kufanya majadiliano na serikali
7th July, 2014
Huku wafuasi wa muungano wa cord wakimiminika katika bustani la uhuru kwa mkutano uliotarajiwa kwa hamu wa sabasaba, vinara wa cord waliamua kutoa mapendekezo ambayo kulingana nao yatasaidia kuleta mabadiliko nchini. Ingawa sabasaba ya mwaka huu ni tofauti kabisa na ile ya waanzilishi wao mwaka 1990, mabadiliko ya uongozi na katiba imekuwa mojawapo ya yale yaliyoongoza mkutano huo.