Usafiri waathirika kutokana na matatu kukosa kuafikiana na sheria za usalama barabarani
1st April, 2014
Maelfu ya wakenya walilazimika kutembea hadi kazini huku wengine wakitumia njia mbadala mapema hii leo, hii ni kufuatia makataa yaliyotolewa kwa magari ya umma yakitakiwa kuafikiana na sheria mpya za kuimarisha usalama barabarani . Miongoni mwa sheria hizo ni pamoja na magari yote ya umma kutakiwa kuwekwa vi9dhibiti mwendo vipya vya kidijitali.