Kuanza kwa matangazo ya digitali yapewa muda zaidi
28th March, 2014
Dijitali au analogi? Mahakama imetoa masharti mapya ambayo imesisitiza ni sharti yazingatiwe kabla ya wakenya kuhama hadi kwenye mfumo wa kupeperusha matangazo ya televisheni kupitia mawimbi ya dijitali. Mwezi wa Septemba mwaka huu ndio muda uliotengwa kwa serikali kuhakikisha kwamba tume ya mawasiliano- CCK, inabuniwa upya kuambatana na katiba iliyoko sasa, kwani tume hiyo kwa sasa haina mamlaka ya kuzima matangazo ya analogi kwa kuwa ilibuniwa kwenye katiba iliyopita.