Mwili wa rubani David Macharia wa patikana bomani kwake
28th February, 2014
Mwili wa mwanamume mmoja uliotambuliwa kama aliyekuwa rubani David Macharia umepatikana katika shimo la maji taka katika boma lake katika mtaa wa Karen. Macharia anasemekana alikuwa ametekwa nyara huku wahalifu hao wakiitaka familia kutoa shilingi laki moja ili kumuachilia. hata hivyo kupatikana kwa mwili wake katika boma lake kumezua maswali zaidi huku polisi wakianzisha uchunguzi kubaini kiini cha kifo chake. Mashirima Kapombe anaarifu.