Spika wa kaunti ya kiambu aondolewa afisini
25th February, 2014
Spika wa kaunti ya kiambu ameondolewa kutoka afisini mwake kwa ukiukaji wa sheria ya kutoa zabuni. Jumla ya wawakilishi sitini na tatu wa wadi waliunga mkono hoja ya kumuondoa mamlakani spika huyo dhidi ya kura kumi na tatu zilizopigwa za kumuunga mkono kuendelea kushikilia wadhifa wa afisa hiyo. Spika huyu ataingia katika vitabu vya historia kama spika wa kwanza wa serikali za kaunti kubanduliwa nje baada ya gavana wa embu Martin Wambora kupitia mfumo uu huu wa kukataliwa na wanachama wa serikali ya kaunti.