Misaada bado haijawafikia waathiriwa wa baa la njaa Turkana
17th February, 2014
Wakazi wa Turkana wanaendelea kuathirika na ukame ambao umesababisha ukosefu wa chakula. Ingawa serikali na mashirika mengine yameingilia kati na kutoa chakula kwa wakaazi wa eneo hilo, wengi wa wakaazi wa vijijini hawajaweza kupata chakula kufuatia hali maya ya miundo mbinu .Huku wengi wakijiuliza serikali imechukuwa hatua ipi kuweza kuokoa maisha ya wakenya wengi wanaoathirika na baa la njaa.