Benki ya cfc stanbic yatoa ufadhili kwa kitengo cha kilimo
5th February, 2014
Benki ya cfc stanbic imetoa ufadhili wa takriban shilingi milioni 2.5 katika kitengo cha kilimo cha tuzo za transform kenya awards 2013
Tuzo hizo ambazo zilianzishwa na shirika la standard group na deloitte kenya zinalenga kuwatambua na kuwatuza wakenya waliojitolewa kuwasaidia wasiojiweza katika jamii. Hundi hiyo ilikabidhiwa afisa mkuu mtendaji wa shirika la habari la Standard Sam Shollei na afisa mkuu mtendaji wa benki ya cfc stanbic Greg Brackenridge.