Wakulima walalamikia gharama ya uzalishaji chai na soko duni
29th January, 2014
Inakisiwa kuwa chai ndio kinywaji maarufu sana hapa Kenya na japo majani chai yanakuzwa katika pembe mbalimbali humu nchini hususan katika maeneo baridi,kiwanda cha chai kinachosaga chai tamu na bora zaidi nchini ni kiwanda cha Gathuthi katika eneo bunge la Tetu katika kaunti ya Nyeri. Chai ya Gathuthi inasifika kwa ubora wake na wakulima zaidi ya 8,000 ambao huvuna majani chai na kuyawasilisha katika kiwanda cha Gathuthi, huzingatia kanuni wanazoagizwa kufuata kuanzia upanzi hadi uvunaji.