Jiji la Nairobi lakabiliwa na uhaba wa magari ya zima moto
26th January, 2014
Kaunti ya Nairobi, inakumbwa na changamoto za ukosefu wa magari ya kuzima moto pindi kunapotokea moto katika mitaa ya jiji la Nairobi. Haya yalibainika usiku wa kuamkia leo baada ya moto kuharibu mali ya wamiliki wa viwanda vidogo katika mtaa wa kariobangi.Na licha wao kujaribu kuwaita zima moto juhudi zao ziliambulia patupu. Seneta wa jiji la Nairobi,alilaumu kwa ufisadi katika afisi za kaunti ya Nairobi kwa kile alichodai licha ya afisi hizo kutoa shilingi milioni 100 za kununua magari ya kisasa kinaya kikuu ni kuwa huduma hizo zimekosekana.