Mkuu wa IMF apongeza Kenya kwa kunawirisha uchumi
7th January, 2014
Mkurugenzi mkuu wa hazina ya fedha ya kimataifa IMF Christine Legarde amepongeza serikali ya Kenya kwa juhudi zake za kunawirisha uchumi.Akizungumza katika ikulu ya rais mjini Mombasa alikomtembelea rais Uhuru Kenyatta, Lagarde ameongeza kuwa shirika lake litazidi kushirikiana na serikali ya Kenya kutimiza malengo yake na marekebisho yanayolenga kukuza maendeleo na uchumi.rais Uhuru Kenyatta kwa upande wake amesema majadiliano kati ya serikali yake na hazina ya fedha duniani yatawezesha uchumi wa kenya kufikia kiwango cha wastani.ziara ya lagarde imefanyika wakati kenya imeshanufaika kutokana na mkopo wa shilingi bilioni 65 kati ya miaka 2011 na 2013 kutoka kwa hazina hiyo.