Wazazi wafurika katika maduka ya jumla kununua vitabu na sare za shule
3rd January, 2014
Baada ya sherehe za krismasi na mwaka mpya wazazi wamo mbioni kuwatayarisha wanao kurudi shuleni kwa muhula wa kwanza.Maduka ya jumla ya kuuza vitabu na sare za shule yalishuhudia foleni za wazazi waliojitokeza kununua bidhaa za wanao.Eneo la Pwani wazazi walifurika katika maduka ya wachuuzi kununua vitabu vilivyotumika wakisema hawawezi kugharamia vitabu madukani.