×
× KTN KTN News KTN Morning Express KTN Leo Leo Mashinani The Big Story Checkpoint News Center E-Paper Lifestyle & Entertainment Nairobian Entertainment Eve Woman Travelog TV Stations KTN Home KTN News KTN Farmers TV Radio Stations Radio Maisha Spice FM Vybez Radio Enterprise VAS E-Learning Digger Classified Jobs Games Crosswords Sudoku The Standard Group Corporate Contact Us Rate Card Vacancies DCX O.M Portal Corporate Email RMS
Login
×
Show Swahili

Msichana aliyekuwa amepotea kwa miaka kumi na miwili apatikana

21st December, 2013

Machozi ya furaha yalitanda katika eneo bunge la kibwezi baada ya msichana aliyekuwa amepotea kwa muda wa miaka kumi na miwili kujiunga na familia yake. Jessica Wanza aliye na umri wa miaka kumi na minne alitoweka mwaka 2001 katika mtaa wa kibera hapa jijini. Anastasia Mukiti, ambaye ni dadake msichana huyo anasema wametumia kila mbinu ikiwemo kutumia ushirikina ili kumpata msichana huyo bila mafanikio. Mamake msichana huyo alifariki mwaka 2003. Mwaka huu hata hivyo waliweka tangazo la kupotea kwa mtoto huyo kupitia shirika la kuwasaidia watoto nchini, na baada ya msichana waliokuwa wakimshuku kufanyiwa uchunguzi ikabainika kuwa alikuwa mtoto ambaye wamekuwa wakimtafuta miaka mingi. Jessica alipatikana katika makao ya watoto ya Nanyuki.
.
RELATED VIDEOS