DRC yatia saini mkataba wa amani na wanamgambo wa M23
13th December, 2013
Nchi ya DRC hapo jana ilipiga hatua ya amani humu nchini Kenya ilipokuwa ikiadhimisha miaka 50 ya uhuru. DRC ilitia saini mkataba na kundi la wanamgambo la M23 katika ikulu ya rais jijini Nairobi. Mkataba ambao unatarajiwa kuleta amani katika nchi hiyo baada ya vita kati ya serikali na wanamgambo hao kuhusu rasilmali. Rais wa malawi Joyce Banda na wa Uganda Yoweri Museveni walisifu pande zote mbili kwa kusikizana na kutoa wito wa kujenga nchi hiyo ili isonge mbele.