Wasichana themanini na wawili wamenusurika ukeketaji huko Masaai Mara
27th November, 2013
Wasichana themanini na wawili kutoka Maasai Mara ambao walitaka kukeketwa na kisha kuozwa wakiwa na umri mdogo wamepata nusura katika shule moja. Mbali na wasichana hao pia wavulana thelathini na watano waliokuwa wakitumika katika kuwapeleka mifugo yao malishoni sasa wana kila sababu ya kutabasamu kwani wanapokea elimu kama watoto wengine.