Rahaeal Wanjala na mpenziwe Akinyi waachiliwa huru
13th November, 2013
Aliyekuwa mbunge wa Budalangi Raphael Wanjala pamoja na anayesemekana kuwa mpenziwe Joyce Akinyi wameachiliwa baada ya kukaa ndani katika kituo cha polisi cha Muthaiga kwa zaidi ya saa 28. Wawili hawa na wengine watatu walikamatwa jana katika eneo la Isinya katika barabara ya kutoka Nairobi kuelekea Namanga , kwa madai ya ulanguzi wa dawa za kulevya. Hata hivyo baada ya uchunguzi mchana mzima, ikabainika walichokuwa wamebeba ni unga. Kisa hiki kinawarejesha katika vicha vya habari, Wanjala na Akinyi baada ya ile sakata yao ya kukamatwa nchini India, kwa madai ya ulanguzi wa dawa za kulevya.