Mtoto akatwa mguu hospitalini
2nd October, 2013
Familia moja mjini Nakuru inaishi kwa majonzi baada ya mtoto wao wa kike aliyezaliwa wiki nane zilizopita, kulazimika kukatwa mguu, katika kile wanakitaja kama utepetevu wa madaktari. Salama waithera alizaliwa katika hospitali ya nakuru nursing home, akiwa salama, lakini wiki moja baadaye akashikwa na homa na ndipo wakamrejesha hospitalini humo. Siku mbili baada ya kupewa dawa, wazazi wa salama wakagundua kuwa mguu wake wa kushoto umeanza kuoza na kugeuka rangi isiyo ya kawaida. Alipelekwa katika hospitali ya kijabe, na jumamosi mguu wake ukakatwa. Wasimamizi wa hospitali hiyo hata hivyo wamejitenga na masaibu ya salama, wakisema ugonjwa uliomuathiri wa kufa kwa seli za neva haukusababishwa na dawa walizompa hospitalini humo.