Ji Cheki na 100 Thao Promotion yaanza rasmi
18th September, 2013
Kampeni ya Jicheki na 100 thao kila siku imeanza rasmi hii leo . Kampeni hiyo itawawezesha wakenya kushinda shilingi laki moja kila siku kwa kununua gazeti la standard. Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi huo uliofanyika hapo jana katika makao makuu ya shirika la Standard Group afisa mkuu mtendaji wa shirika la habari la Standard Group Sam Shollei amesema kampeni hiyo inalenga kuwashukuru wateja wake kwa ushirikiano wao kwa miaka zaidi ya 100. Kampeni hiyo imeanza leo hii na itakamilika tarehe mosi mwezi Novemba mwaka huu huku droo ya mwisho ikifanyika tarehe 2 mwezi wa Novemba.