Jaji David Majanja kutupilia mbali rufaa ya kupinga ushindi wa Daktari Alfred Mutua
17th September, 2013
Jaji David Majanja ametupilia mbali rufaa ya kupinga ushindi wa Daktari Alfred Mutua kama Gavana wa kaunti ya Machakos .kwenye uamuzi wake jaji majanja amesema kuwa mlalamishi kwenye kesi hiyo, aliyekuwa waziri wa masuala ya vijana Wavinya Ndeti hakutoa ushahidi wa kutosha wa kuthibitisha madai yake. Ndeti alikuwa ameitaka mahakama kutupilia mbali ushindi wa Mutua akidai kuwa kura zilizopigwa zilizidi idadi ya wapiga kura. Aidha alisema kuwa Mutua aliweka mabango ya picha zake za kampeni kwenye barabara, na njia zilizoelekea katika vituo vya kupigia kura hadi siku ya uchaguzi. Alisema hatua hiyo ilikiuka sheria ya uchaguzi. Hata hivyo jaji majanaja amesema hapakuwa na ushahidi wa kuthibitisha madai hayo mbali na kumtaka wavinya ndeti kulipa gharama za kesi hiyo