Mpenzi wa Bibi wa Tuju, Tony Ogunda afariki
2nd July, 2013
Mwanamume aliyeshtumiwa kuhusika kimapenzi na mkewe aliyekuwa waziri Raphael Tuju amepatikana amefariki. Maafisa wa polisi wanasema kuwa mwili wa tony ogunda ulipatikana katika nyumba moja iliyopo katika eneo la Upper Hill hapa Nairobi. Rafikiye amewaeleza polisi kuwa Ogunda alikuwa katika mkahawa mmoja eneo la River Road usiku wa kuamkia leo ,kabla ya kwenda kwake. Mkuu wa polisi eneo la nairobi Benson Kibui amekitaja kifo chake kuwa cha ghafla.