Balozi wa Slovakia azuru Standard Group
13th June, 2013
Taifa la Kenya huenda likasaidika pakubwa kufuatia uwekezaji kutoka kwa taifa la Slovakia humu nchini kama njia moja ya kuimarisha uchumi wa Kenya. katika ziara yake katika shirika la habari la Standard alasiri ya leo, balozi wa Slovakia humu nchini Michal Mlynar amesema kuwa wameanzisha kampuni ya kusaga plastiki na kutengeneza bidhaa mbalimbali ikiwemo kawi, mjini kisumu inayotarajiwa kutoa ajira kwa zaidi ya wakenya elfu mbili.