Buriani kwa Bi Kidude
17th April, 2013
Gwiji na mkongwe wa nyimbo za taarab na za unyagoni Fatuma Binti Baraka maarufu kama Bi Kidude ameaga dunia hii leo . Bi Kidude ambaye licha ya umri wake mkubwa alikuwa bado akiendelea kushiriki kwenye tamasha mbalimbali za muziki alifariki hii leo nyumbani kwake katika kijiji cha Raha Leo, kisiwani Zanzibar. Mwanahabari Saida Swaleh na mengi kuhusu safari ya mutribu huyo aliyejizolea sifa tele afrika mashariki na kote ulimwenguni.