Vikwazo kwa Kenya kuhusu uchaguzi
14th February, 2013
Suala la ICC na uchaguzi mkuu utakaofanyika machi 4, huezi litenganisha na limekuwa kama chanda na pete. Na limetokota zaidi pale semi kutoka mataifa ya magharibi zimetafsiriwa kana kwamba kenya itajipata matatani iwapo ndoto ya uhuru kenyatta na william ruto wanaokabiliwa na mashtaka ya jinai, huko the hague itatimia na kuingia ikulu. Rais wa Marekani Barack Obama, katika ujumbe wa kenya obama alisema marekani haimshabikii mgombeaji yeyote, chaguo la wakenya ni lao wenyewe. Lakini siku kadhaa baadaye balozi wa marekani anayehusika na masuala ya afrika johnnie carson pamoja na mabalozi wa umoja wa ulaya walionekana kugusia kuwa huenda kukawa na athri iwapo kenya itawachagua watu fulani………na ndio mkoko umeanza kualika maua? Je kuna tishio la kenya kuwekewa vikwazo iwapo itawachagua uhuru na ruto?