Mauaji Ikolomani
13th February, 2013
Kijiji kimoja kaunti ya kakamega kimegubikwa na huzuni na mshtuko baada jamaa mmoja kuwaua watoto wake 3, kumjeruhi mkewe na kisha kujiua.kiwingu cheusi kulitanda katika kijiji cha irichero eneo bunge la ikolomani, baada ya wenyeji kuamkia taarifa hizo za kuhuzunisha za mauaji ya watoto hao mmoja akiwa malaika wa miezi 2 unusu. Inadaiwa bwana huyo aliacha notisi iliosema kwamba alikua ameathirika na ukimwi na hakutaka familia yake iteseke atakapofariki.