News: Mtoto aliyetekwa nyara aokolewa
1st February, 2013
Visa vya utekaji nyara vinaendelea kuripotiwa kila uchao kote nchini ambapo huko kitengela viungani mwa jiji la nairobi, polisi wamemuokoa mvulana wa miaka 2 kutoka mikononi mwa majangili waliomteka nyara nyakati za mchana.kijana huyo alitekwa nyara walipokua na kijakazi wao wa nyumbani katika matembezi hapo juzi. Polisi iliweza kuwakamata washukiwa hao ambao walikua pamoja na kijakazi huyo ambaye alitengeza mpango huo.