Junaa la NHIF
9th August, 2012
Kaimu afisa mkuu mtendaji wa nhif Adan Adan amekana madai ya kuhusishwa na ajira ya jamaa zake akiwemo mkewe. Katika taarifa kwa vyombo vya habari alitaja shinikizo kutoka nje kuwa mwanzo wa njama ya kutibua usimamizi huo ulioteuliwa baada ya ule wa kwanza kuondolewa kwa madai ya ufujaji wa fedha. Wakati huo huo aliyekuwa afisa mtendaji wa NHIF Richard Rerich leo alihojiwa katika tume ya kupambana na ufisadi.